


Historia Fupi
Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA) ni muungano wa Taasisi mbili zilizokuwa na mamlaka kamili za kiutendaji, ofisi zenyewe ni Ofisi ya Mrajisi wa Vizazi na Vifo na Ofisi ya Usajili na Kadi za Utambulisho Zanzibar. Ofisi hii imeanzishwa kwa Sheria Namba 3 ya 2018, ina majukumu ya kusajili Matukio ya kijamii na kutoa vyeti maalum, matukio hayo ni Vizazi, Vifo, Ndoa, Talaka na Vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi na Wasiokua Wazanzibari Wakaazi.
- Vizazi
- Ndoa
- Talaka
- Vifo
- Utambulisho
Kimuundo Ofisi ya Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii inaongozwa na Bodi ya Ushauri ya Wakala chini ya Mwenyekiti wa Bodi hiyo na Mkurugenzi Mtendaji ambaye ameteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi