


Historia Fupi
Wakala wa Usajili wa matukio ya Kijamii Zanzibar ni muungano wa Taasisi mbili zilizokuwa na mamlaka kamili za kiutendaji, ofisi zenyewe ni Afisi ya Vizazi na Vifo na Afisi ya Usajili na Kadi za Utambulisho Zanzibar. Afisi hii imeanzishwa kwa Sheria Namba 3 ya 2018, ina majukumu ya kusajili Matukio ya kijamii na kutoa vyeti maalum, matukio hayo ni Vizazi, Vifo, Ndoa, Talaka na Vitambulisho vya Mzanzibari Mkaazi na wasiyokua Wazanzibari Wakaazi.
- Vizazi
- Ndoa
- Talaka
- Vifo
- Utambulisho
Afisi ya Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii inaongozwa na Bodi ya Ushauri chini ya Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mtendaji ambae ameteuliwa na Rais wa Zanzibar na Baraza la Mapinduzi